Friday, May 20, 2011

IJUE KARAFUU

 KARAFUU......



tunajua ya kwamba karafuu ni zao linalonukia saaana na tena harufu yake ni nzuri sana sasa jamani kuna watu fulani siku hizi wanasema mwanamke ama mwanaume shurti uogeshwe na karafuu ama iliki ili unukie vizuri na kumvutia mpenzi wako haya mambo zamani yalikuwa yanafanywa na watu wa pwani lakini siku hizi kila kabila bibi lina manjonjo...

kwa mimi binafsi harufu ya karafuu ama iliki naipenda tu kwenye chakula lakini kwenye mwili wa mpenzi wangu wala sitaki kuisikia, na kwa wengine ambao wapo kama mimi wasiopenda harufu kuna vitu vyengine ambavyo vinaweza kuchukuwa nafasi ya karafuu na iliki kama udi wa vanilla, roses, ama hata wa lily flower.. manukato hayo unayachoma kwenye kifukizo na kuyaweka chumbani kwangu kuliko hiyo harufu kali ya karafuu (huu ni kwa upande wangu)...

na kabla mwanamke hujaamua kuweka hizo karafuu na iliki kumpendezesha mpenzi wako hebu muulize kwanza maana usije ukanunua ukaweka chumbani kumbe mwenzako badala aingie ndani anakimbia chumba, itakuwa aibu...

wote tunapenda chumbani kwetu panukie vizuri lakini wapenzi wetu huwa wana matatizo na harufu iwe nzuri ama mbaya wao kutwa na chafya, mafua mpaka utawaonea huruma...

kwahiyo tusijifanye tunaujua ufundi hebu kabla ya kumuwekea mpenzi mankodinkodi hebu tuulize tujuwe kipi kina faa na kipi hakifai....

MFAIDISHE MWENZI WAKO

 MDALASINI, TANGO NA ASALI....

jamani wenzangu nina jambo mlikuwa mnajua kama mdalasini, asali na tango ni dawa ya kumpa mtu nguvu kwenye mechi? kama ulikuwa hujui ndio ufahamu eti..


kuna dada mmoja alikuwa analalamika mpenzi wake nguvu kitandani hana, anasema jamaa akishatoa moja tu basi nguvu zote zinaisha jamaa hawezi hata kurudia ya pili, na hapo mwanamke wake huyo anakuwa hajatosheka lakini jamaa hajiwezi kabisa..




sasa huyu dada akawa anaomba ushauri kwa watu wazima akiwaeleza swala lake na mumewe watu wengi wakawa wanamshauri mengi tu pamoja na ya kwamba mumewe anywe maji ya mchele yale ya kwanza, sijui mwengine akamwambia anywe maji ya madafu kwa wingi na wengine wakimwambia aende kutafuta dawa za miti shamba...



akafika kwa bibi mmoja wa zamani (umri umeenda) yule bibi akamwambia yule dada ampe mumewe mdalasini pamoja na asali achanganye kwa pamoja atie na maji ama aiweke kwenye chai, halafu kila chakula cha yule baba kisikose kipande cha tango..



yule dada akafanya kama alivyoambiwa na yule bibi, sasa hivi dada anafuraha mambo si shwari, kwahiyo huu ni ushauri tu ya kwamba ukiona mwezio nguvu hana akienda moja anahema kama kasukuma trekta, mwanaume anahema kama presha imeshuka (hehehe) basi sio vibaya ukijaribu hayo..



lakini naomba niseme sio tu kwasababu huyu dada yeye mpenzi wake alipata nafuu ndio kila mtu itakuwa hivyo wengine vyao vya kurithi utalisha hivyo vitu milele jamaa hata kubadilika asibadilike...BY KHADIL HEMED KANTANGAYO